Wednesday, July 31, 2013

  Umepanda meli na humo kwenye meli mpo watu wengi baadhi ni abiria tu wanaosafirishwa na wengine ni sehemu ya mabaharia wanaohakikisha meli inafika inakoelekea. Ghafla hali ya bahari inabadilika na meli inayumba sana na ili kuweza kuendelea na safari inabidi baadhi ya watu watoswe majini ili kupunguza uzito. Unafikiri ni watu gani watakaotoswa majini? Abiria ama baharia?



  Sote tunakubali kwamba watakaotoswa majini ni abiria. Hakuna anaeweza hata kufikiria kwamba baharia atoswe majini. Kwa nini baharia asitoswe na abiria wengine waweze kutoswa? Wote si ni binadamu sawa? Katika hali kama hiyo kinachojalisha sio ubinadamu bali umuhimu. Baharia anaachwa kwa sababu yeye ni wa muhimu kwenye chombo kuliko abiria wa kawaida.
  Jiulize wewe je kwenye meli uliyopanda wewe ni abiria wa kawaida ama sehemu ya mabaharia?
  Kwenye maisha yako kuna meli nyingi ulizopanda, baadhi ya meli hizo ni ajira, na nafasi mbali mbali kwenye jamii.
  Kwa mfano kwenye ajira kama kampuni ama shirika unalofanya kazi likipata msukosuko na kuhitaji kupunguza wafanyakazi watakaoanza kupunguzwa ni wale ambao hawana umuhimu mkubwa kwa shirika. Yaani watapunguzwa wale ambao ni mzigo, ambao hata wasipokuwepo hakuwezi kuwa na athari kubwa sana.



  Jitafakari kwenye ajira yako wewe ni baharia ama abiria? Je kuna kipi cha muhimu sana ambacho kampuni ama shirika linapata kutoka kwako. Je ni rahisi tu kwa wewe kupunguzwa ama kufukuzwa?
  Sio lazima uwe mkurugenzi ama injinia mkuu ndio uwe wa muhimu sana kwenye sehemu yako ya kazi. Hata kama wewe ni mfanya usafi tu unaweza kuamua kuwa wa muhimu sana kiasi kwamba sio rahisi kwa wewe kuondolewa. Kwa sababu hata wapunguzwe wafanyakazi kwa asilimia 70 bado lazima atabakishwa mfanya usafi japo mmoja. Unafikiri kitatumika kigezo gani kumbakisha huyo mmoja?
  Kwenye kitengo chochote unachofanya kazi unaweza kuwa wa muhimu sana na kufanya iwe ngumu kuondolewa kirahisi.
  Ili uwe wa muhimu ni lazima kile unachofanya ufanye kwa utofauti na kwa kiwango cha hali ya juu. Ni rahisi kwako kuweza kufanya hivyo kama utatumia uwezo na vipaji vya pekee ulivyonavyo.
  Hakikisha chochote unachofanya unaleta mabadiliko kwako na kwa wanaokuzunguka. Mabadiliko hayo yatakufanya uwe wa pekee na kuwa wa muhimu kwenye kazi unayofanya.

JE WEWE NI BAHARIA AMA ABIRIA?

  Umepanda meli na humo kwenye meli mpo watu wengi baadhi ni abiria tu wanaosafirishwa na wengine ni sehemu ya mabaharia wanaohakikisha meli inafika inakoelekea. Ghafla hali ya bahari inabadilika na meli inayumba sana na ili kuweza kuendelea na safari inabidi baadhi ya watu watoswe majini ili kupunguza uzito. Unafikiri ni watu gani watakaotoswa majini? Abiria ama baharia?



  Sote tunakubali kwamba watakaotoswa majini ni abiria. Hakuna anaeweza hata kufikiria kwamba baharia atoswe majini. Kwa nini baharia asitoswe na abiria wengine waweze kutoswa? Wote si ni binadamu sawa? Katika hali kama hiyo kinachojalisha sio ubinadamu bali umuhimu. Baharia anaachwa kwa sababu yeye ni wa muhimu kwenye chombo kuliko abiria wa kawaida.
  Jiulize wewe je kwenye meli uliyopanda wewe ni abiria wa kawaida ama sehemu ya mabaharia?
  Kwenye maisha yako kuna meli nyingi ulizopanda, baadhi ya meli hizo ni ajira, na nafasi mbali mbali kwenye jamii.
  Kwa mfano kwenye ajira kama kampuni ama shirika unalofanya kazi likipata msukosuko na kuhitaji kupunguza wafanyakazi watakaoanza kupunguzwa ni wale ambao hawana umuhimu mkubwa kwa shirika. Yaani watapunguzwa wale ambao ni mzigo, ambao hata wasipokuwepo hakuwezi kuwa na athari kubwa sana.



  Jitafakari kwenye ajira yako wewe ni baharia ama abiria? Je kuna kipi cha muhimu sana ambacho kampuni ama shirika linapata kutoka kwako. Je ni rahisi tu kwa wewe kupunguzwa ama kufukuzwa?
  Sio lazima uwe mkurugenzi ama injinia mkuu ndio uwe wa muhimu sana kwenye sehemu yako ya kazi. Hata kama wewe ni mfanya usafi tu unaweza kuamua kuwa wa muhimu sana kiasi kwamba sio rahisi kwa wewe kuondolewa. Kwa sababu hata wapunguzwe wafanyakazi kwa asilimia 70 bado lazima atabakishwa mfanya usafi japo mmoja. Unafikiri kitatumika kigezo gani kumbakisha huyo mmoja?
  Kwenye kitengo chochote unachofanya kazi unaweza kuwa wa muhimu sana na kufanya iwe ngumu kuondolewa kirahisi.
  Ili uwe wa muhimu ni lazima kile unachofanya ufanye kwa utofauti na kwa kiwango cha hali ya juu. Ni rahisi kwako kuweza kufanya hivyo kama utatumia uwezo na vipaji vya pekee ulivyonavyo.
  Hakikisha chochote unachofanya unaleta mabadiliko kwako na kwa wanaokuzunguka. Mabadiliko hayo yatakufanya uwe wa pekee na kuwa wa muhimu kwenye kazi unayofanya.

Posted at Wednesday, July 31, 2013 |  by Makirita Amani

0 comments:

USIACHE KUWEKA MAONI YAKO HAPA.

  Unaamka asubuhi unaelekea kwenye shughuli zako, unafanya kazi, unarudi nyumbani, unapumzika na kuangalia tv ama kuingia kwenye mitandao ya kijamii, unakula, unaenda kulala. Kesho tena unafanya hivyo hivyo na unarudia hivyo kwa sehemu kubwa ya maisha yako.

routine5routine2

  Kwenye maisha yako kuna vitu unavifanya mara kwa mara na unavifanya kwa mbinu na mtindo ule ule kila mara. Inaweza kuwa kwenye maisha ya kawaida, kwenye kazi ama hata jinsi ya kufikiri.

routine

  Ni vizuri kuwa na utaratibu ama mpangilio wa maisha ila haimaanishi maisha yawe kama amri isiyobadilishwa. Kuishi maisha yale yale kwa kufanya vitu vile vile kia siku inapunguza uwezo wa kufkiri na ugunduzi.

  Ni vigumu sana kupata mawazo mapya ama kugundua kitu kipya kwa kufanya yale yale unayofanya kila siku na kwa mtindo ule ule unaofanyia.

  Pia kufanya mambo mara kwa mara kwa njia moja tu ni chanzo mojawapo cha msongo wa mawazo.

routine4

Baadhi ya mambo unayoweza kuyabadili leo na uanze kufurahia maisha ni haya;

  Kama kila siku unakwenda kwenye shughuli zako kwa kupita njia moja basi leo jaribu kupita njia tofauti. Hakikisha unapita njia tofauti tofauti kila siku kwa sababu unavyoviona vinaweza kubadili mtizamo wako. Kama unaona vile vile kila siku hata mtizamo wako unakuwa vile vile.

  Kama huwa unakwenda kwenye shughuli zako za kila siku kwa kutumia usafiri wako binafsi siku moja moja panda usafiri wa jumuia(daladala). Kuna mengi sana utajifunza humo ambayo ni vigumu sana kuyapata ukiwa kwenye gari lako mwenyewe.

daladalagari

  Kama unafanya kazi ofisini na unakaa meza ile ile na kiti kiko sehemu ile ile kila siku leo badili hata mpangilio wa kiti. Kwa kukaa tu tofauti na kila siku unavyokaa kunachochea kutafakari kwa utofauti.

  Angalia njia tofauti unayoweza kufanya kazi yako ama kutoa huduma yako. Kwa kuwa na utofauti kutakufanya uifurahie kazi yako na hata wale unaowafanyia kazi ama kuwapa huduma watafurahishwa pia.

Binadamu hatupaswi kuwa kama ‘robot’ lazima tuyabadili mazingira yanayotuzunguka ile tuweze kuwa na furaha na pia kuwa wabunifu. Jitahidi kubadili kila unachoona kinaweza kubadilika kwenye maisha yako.

SIO LAZIMA KILA SIKU IWE HIVI…

  Unaamka asubuhi unaelekea kwenye shughuli zako, unafanya kazi, unarudi nyumbani, unapumzika na kuangalia tv ama kuingia kwenye mitandao ya kijamii, unakula, unaenda kulala. Kesho tena unafanya hivyo hivyo na unarudia hivyo kwa sehemu kubwa ya maisha yako.

routine5routine2

  Kwenye maisha yako kuna vitu unavifanya mara kwa mara na unavifanya kwa mbinu na mtindo ule ule kila mara. Inaweza kuwa kwenye maisha ya kawaida, kwenye kazi ama hata jinsi ya kufikiri.

routine

  Ni vizuri kuwa na utaratibu ama mpangilio wa maisha ila haimaanishi maisha yawe kama amri isiyobadilishwa. Kuishi maisha yale yale kwa kufanya vitu vile vile kia siku inapunguza uwezo wa kufkiri na ugunduzi.

  Ni vigumu sana kupata mawazo mapya ama kugundua kitu kipya kwa kufanya yale yale unayofanya kila siku na kwa mtindo ule ule unaofanyia.

  Pia kufanya mambo mara kwa mara kwa njia moja tu ni chanzo mojawapo cha msongo wa mawazo.

routine4

Baadhi ya mambo unayoweza kuyabadili leo na uanze kufurahia maisha ni haya;

  Kama kila siku unakwenda kwenye shughuli zako kwa kupita njia moja basi leo jaribu kupita njia tofauti. Hakikisha unapita njia tofauti tofauti kila siku kwa sababu unavyoviona vinaweza kubadili mtizamo wako. Kama unaona vile vile kila siku hata mtizamo wako unakuwa vile vile.

  Kama huwa unakwenda kwenye shughuli zako za kila siku kwa kutumia usafiri wako binafsi siku moja moja panda usafiri wa jumuia(daladala). Kuna mengi sana utajifunza humo ambayo ni vigumu sana kuyapata ukiwa kwenye gari lako mwenyewe.

daladalagari

  Kama unafanya kazi ofisini na unakaa meza ile ile na kiti kiko sehemu ile ile kila siku leo badili hata mpangilio wa kiti. Kwa kukaa tu tofauti na kila siku unavyokaa kunachochea kutafakari kwa utofauti.

  Angalia njia tofauti unayoweza kufanya kazi yako ama kutoa huduma yako. Kwa kuwa na utofauti kutakufanya uifurahie kazi yako na hata wale unaowafanyia kazi ama kuwapa huduma watafurahishwa pia.

Binadamu hatupaswi kuwa kama ‘robot’ lazima tuyabadili mazingira yanayotuzunguka ile tuweze kuwa na furaha na pia kuwa wabunifu. Jitahidi kubadili kila unachoona kinaweza kubadilika kwenye maisha yako.

Posted at Wednesday, July 31, 2013 |  by Makirita Amani

0 comments:

USIACHE KUWEKA MAONI YAKO HAPA.

Tuesday, July 30, 2013

  Kuna mijadala mingi kuhusu nani anaweza kuwa mjasiriamali na kuweza kufanikiwa. Kuna wanaosema wajasiriamali huzaliwa na wengine wanasema wajasiriamali wanatengenezwa.

  Wanaosema wajasiriamali wanazaliwa wanaamini kwamba tabia za kijasiriamali mtu anazaliwa nazo na wala sio kujifunza. Wanaamini kwamba kwa wanaoingia kwenye ujasiriamali na kushindwa ni kwa sababu hawajazaliwa na tabia ya ujasiriamali. Kwamba hata wakikazana kwa kiasi gani bado hawana kile kinachohitajika ili kufanikiwa kwenye ujasiriamali.

mjasiriamali

  Kwa wanaosema wajasiriamali wanatengenezwa, wanaamini mtu anaweza kufundishwa na kuwa mjasiriamali. Wanaamini mtu akipewa mafunzo mazuri ya ujasiriamali anaweza kuwa mjasiriamali mzuri na kufanikiwa sana.

mjasiriamali2

  Kabla ya kusema moja kwa moja ni wazo lipi hapo ni sahihi na ni lipi hapo sio sahihi kwanza tuangaie tabia za binadamu kiujumla na tabia za wajasiriamai.

  Mjasiriamali ni mtu anaejiamini, mwenye ndoto na mwenye ujasiri wa hali ya juu.

  Kuweza kuanza ujasiriamali kunahitaji kujiamini kwa hali ya juu na kuweza kufanya mambo ya hatari(kutake risk) kunahitaji ujasiri mkubwa. Na ili aweze kundelea mbele licha ya matatizo unayokumbana nayo ni lazima mjasiriamai awe na ndoto na maengo makubwa aliyojiwekea.

  Tabia hizo tatu kuu za ujasiriamali hakuna anaezaliwa nazo ila tunazipata kutoka kwenye mazingira tunayokulia na tunayoishi mara nyingi.

  Mtoto aliekulia kwenye familia ama jamii inayomjengea kujiamini moja kwa moja naye atajiamini. Mtoto aliekulia kwenye jamii ya watu wanaotake risk moja kwa moja nae atajenga tabia hiyo. Kwa kifupi tabia zinaambukizwa. Ndio maana unaweza kuona baadhi ya makabila ni wafanya biashara maarufu wakati kuna baadhi ya makabila wanapenda kazi ndogondogo.

  Sio kwamba kuna mbegu moja kwenye kabila fulani na mbegu nyingine kwenye kabila jingine, hapana, kinachotokea ni kuambukizana tabia. Kumbuka wanaokuzunguka wana mchango mkubwa sana wa hapo ulipofikia.

  Hivyo basi kuchukulia uambukizano huu wa tabia kama tabia za kuzaliwa tunaweza kujumuisha kwamba wajasiriamali huzaliwa. Je hii ina maana kama mtu hajakaa kwenye mazingira yanayoweza kumuambukiza tabia hizo hawezi kuwa mjasiriamali?

  Mtu yeyote, narudia tena yeyote anaweza kuwa mjasiriamali kama tu atafanya MAAMUZI. Kikubwa kinachopima kufanikiwa ama kutofanikiwa kwa mjasiriamali ni maamuzi. Mtu yeyote anaeamua kwa moyo mmoja kwamba maisha yake sasa ni ujasiriamali na hakuna kitakachomtoa kwenye maisha hayo anauwezekano mkubwa sana wa kufanikiwa katika ujasiriamali.

  Mtu akishafanya maamuzi thabiti moja kwa moja ataanza kutafuta njia za kufanikiwa kwenye ujasiriamali na hapo ndipo atajifunza tabia za kuweka ndoto na maengo makubwa, ujasiri, kujiamini na kufanya mambo ya hatari.

  Tusiubeze uwezo wa akili na maamuzi ya binadamu, binadamu anauwezo mkubwa sana wa kufanya chochote anachoweza kukifikiria kwenye akili yake.

mjasiriamali3

  Fanya maamuzi sasa ya kuwa mjasiriamali na uyamiliki maisha yako. Usiogopeshwe na waliokuzunguka ama historia ya familia yako. Wewe ni wa pekee na una uwezo mkubwa sana wa kueta mabadiliko. Ukifanya maamuzi ambayo hayatetereki lazima utafikia ndoto na maengo yako. Hakuna anaekujua wewe zaidi ya wewe mwenyewe. Tumia uwezo na vipaji vyako kuleta mabadiliko kwako na kwa jamii inayokuzunguka.

WEWE NI MJASIRIAMALI PALE TU UTAPOFANYA HIVI

  Kuna mijadala mingi kuhusu nani anaweza kuwa mjasiriamali na kuweza kufanikiwa. Kuna wanaosema wajasiriamali huzaliwa na wengine wanasema wajasiriamali wanatengenezwa.

  Wanaosema wajasiriamali wanazaliwa wanaamini kwamba tabia za kijasiriamali mtu anazaliwa nazo na wala sio kujifunza. Wanaamini kwamba kwa wanaoingia kwenye ujasiriamali na kushindwa ni kwa sababu hawajazaliwa na tabia ya ujasiriamali. Kwamba hata wakikazana kwa kiasi gani bado hawana kile kinachohitajika ili kufanikiwa kwenye ujasiriamali.

mjasiriamali

  Kwa wanaosema wajasiriamali wanatengenezwa, wanaamini mtu anaweza kufundishwa na kuwa mjasiriamali. Wanaamini mtu akipewa mafunzo mazuri ya ujasiriamali anaweza kuwa mjasiriamali mzuri na kufanikiwa sana.

mjasiriamali2

  Kabla ya kusema moja kwa moja ni wazo lipi hapo ni sahihi na ni lipi hapo sio sahihi kwanza tuangaie tabia za binadamu kiujumla na tabia za wajasiriamai.

  Mjasiriamali ni mtu anaejiamini, mwenye ndoto na mwenye ujasiri wa hali ya juu.

  Kuweza kuanza ujasiriamali kunahitaji kujiamini kwa hali ya juu na kuweza kufanya mambo ya hatari(kutake risk) kunahitaji ujasiri mkubwa. Na ili aweze kundelea mbele licha ya matatizo unayokumbana nayo ni lazima mjasiriamai awe na ndoto na maengo makubwa aliyojiwekea.

  Tabia hizo tatu kuu za ujasiriamali hakuna anaezaliwa nazo ila tunazipata kutoka kwenye mazingira tunayokulia na tunayoishi mara nyingi.

  Mtoto aliekulia kwenye familia ama jamii inayomjengea kujiamini moja kwa moja naye atajiamini. Mtoto aliekulia kwenye jamii ya watu wanaotake risk moja kwa moja nae atajenga tabia hiyo. Kwa kifupi tabia zinaambukizwa. Ndio maana unaweza kuona baadhi ya makabila ni wafanya biashara maarufu wakati kuna baadhi ya makabila wanapenda kazi ndogondogo.

  Sio kwamba kuna mbegu moja kwenye kabila fulani na mbegu nyingine kwenye kabila jingine, hapana, kinachotokea ni kuambukizana tabia. Kumbuka wanaokuzunguka wana mchango mkubwa sana wa hapo ulipofikia.

  Hivyo basi kuchukulia uambukizano huu wa tabia kama tabia za kuzaliwa tunaweza kujumuisha kwamba wajasiriamali huzaliwa. Je hii ina maana kama mtu hajakaa kwenye mazingira yanayoweza kumuambukiza tabia hizo hawezi kuwa mjasiriamali?

  Mtu yeyote, narudia tena yeyote anaweza kuwa mjasiriamali kama tu atafanya MAAMUZI. Kikubwa kinachopima kufanikiwa ama kutofanikiwa kwa mjasiriamali ni maamuzi. Mtu yeyote anaeamua kwa moyo mmoja kwamba maisha yake sasa ni ujasiriamali na hakuna kitakachomtoa kwenye maisha hayo anauwezekano mkubwa sana wa kufanikiwa katika ujasiriamali.

  Mtu akishafanya maamuzi thabiti moja kwa moja ataanza kutafuta njia za kufanikiwa kwenye ujasiriamali na hapo ndipo atajifunza tabia za kuweka ndoto na maengo makubwa, ujasiri, kujiamini na kufanya mambo ya hatari.

  Tusiubeze uwezo wa akili na maamuzi ya binadamu, binadamu anauwezo mkubwa sana wa kufanya chochote anachoweza kukifikiria kwenye akili yake.

mjasiriamali3

  Fanya maamuzi sasa ya kuwa mjasiriamali na uyamiliki maisha yako. Usiogopeshwe na waliokuzunguka ama historia ya familia yako. Wewe ni wa pekee na una uwezo mkubwa sana wa kueta mabadiliko. Ukifanya maamuzi ambayo hayatetereki lazima utafikia ndoto na maengo yako. Hakuna anaekujua wewe zaidi ya wewe mwenyewe. Tumia uwezo na vipaji vyako kuleta mabadiliko kwako na kwa jamii inayokuzunguka.

Posted at Tuesday, July 30, 2013 |  by Makirita Amani

1 comments:

USIACHE KUWEKA MAONI YAKO HAPA.

  Kwa mfano nikikupigia simu sasa hivi na kukuambia kwamba nahitaji kukaa na wewe kwa saa moja na unielekeze kuhusu jambo fuani linalohusiana na unachofanya utaniambia nikupe shilingi ngapi? Je unajua saa yako moja ina gharama ya shilingi ngapi? Kwa wengi ni ngumu sana kujibu hilo swali. Unaweza kujitetea kwamba kwa kazi unayofanya huwezi kujua gharama ya saa yako moja, ila sio kweli. Kwa kazi yoyote unayofanya hata kama ni kilimo kila saa, dakika na hata sekunde yako ina gharama.

timemoney

  Kama mpaka sasa hujui gharama ya saa yako moja ni vyema ukajifunza hapa ili uweze kujua kwa sababu ni muhimu sana kwa wewe kufikia malengo yako. Ni lazima ujue gharama ya muda wako ili usiutumie tu hovyo.

  Sote tunajua kwamba ni lazima kuwa na malengo kwenye maisha na kwamba malengo yamegawanyika kwenye makundi mbalimbali. Kundi mojawapo la malengo ni malengo ya kifedha.

  Ili kuweza kujua gharama ya muda wako kwanza ni lazima uwe na maengo ya kifedha. Kwa mfano kama lengo lako ni kupata shilingi milioni ishirini(tsh 20,000,000/=) ndani ya mwaka mmoja ujao ni rahisi kujua saa yako moja itagharimu shiingi ngapi.

wekundu

Mwaka mmoja una wiki hamsini na mbili(52), tukindoa wiki nne za kupumzika ama likizo zinabaki wiki 48 za kufanya kazi. Wiki moja ina siku tano za kufanya kazi(hiki ni kiwango cha chini kuna wengine wana siku 6 au 7) kwa kutumia siku tano za wiki kwa wiki 48 utakuwa na siku 240 za kufanya kazi kwa mwaka.

  Siku moja ina masaa nane(8) ya kufanya kazi, hichi pia ni kiwango kidogo ila kuna wenye mpaka masaa 12 ya kufanya kazi kwa siku. kwenye siku 240 za kazi kwa mwaka utakuwa na masaa 1920 ya kufanya kazi kwa mwaka.

  Ukigawanya milioni 20 unazotaka kupata kwa mwaka kwa masaa 1920 ya kufanya kazi unapata shilingi 10, 416/=. Kwa hiyo kwa hesabu za karibu ni shilingi  elfu kumi kwa saa.

  Hivyo kama unataka kutengeneza shilingi milioni ishirini(20,000,000/=) kwa mwaka inabidi kila saa (katika masaa nane ya kufanya kazi kwa siku) uitengeneze shilingi elfu kumi(10,000/=).

PESA TZ

Hayo ni mahesabu kwa kiwango hich cha hela ila unaweza kufanya kulingana na kiwango unachotaka wewe inaweza kuwa pungufu ya hapo ama zaidi ya hapo.

  Pia katika hesabu zako ni vyema kutenga muda wa dharura kwa mambo yatakayojitokeza yatakayoweza kusababisha usifanye kazi, kwa mfano magonjwa ama misiba ya watu wa karibu. Sio muda mwingi sana hivyo kama unatumia zaidi ya saa nane kwa siku kufanya kazi(na ni lazima kufanya hivyo kama unataka kuleta tofauti) bado hesabu zitakuwa sawa na hizo.

  Unafanya nini pale ambapo huna kazi ya kufanya?

  Unaweza kuwa umeshafanya hesabu zako na kupata gharama za muda wako. Ila kwa sasa huna kazi unayofanya ili kuingiza kipato hicho kwa saa! Ama unaweza kusema kwa kuwa sasa huna kazi ama biashara unayofanya hivyo huna haja ya kufanya hesabu hizo!

  Hata kama kwa sasa huna kazi unayofanya, ni muhimu kufanya hesabu hizo kwa kuwa tayari una malengo ya kufikia hatua fuani. Baada ya kujua gharama zako basi hakikisha kila saa unaitumia kukuweka kwenye mazingira ya kupata kiasi ulichopanga. Kama gharama ya saa yako moja ni shilingi elfu kumi basi kila unachofanya kikuweke kwenye mazingira ya kuja kutengeneza hiyo elfu kumi ama zaidi. Inaweza kuwa kwa kuendelea kujifunza, ama kutengeneza mtandao wa watu amba ni muhimu kwa ujuzi ulionao.

UNAJUA THAMANI YA MUDA WAKO?

  Kwa mfano nikikupigia simu sasa hivi na kukuambia kwamba nahitaji kukaa na wewe kwa saa moja na unielekeze kuhusu jambo fuani linalohusiana na unachofanya utaniambia nikupe shilingi ngapi? Je unajua saa yako moja ina gharama ya shilingi ngapi? Kwa wengi ni ngumu sana kujibu hilo swali. Unaweza kujitetea kwamba kwa kazi unayofanya huwezi kujua gharama ya saa yako moja, ila sio kweli. Kwa kazi yoyote unayofanya hata kama ni kilimo kila saa, dakika na hata sekunde yako ina gharama.

timemoney

  Kama mpaka sasa hujui gharama ya saa yako moja ni vyema ukajifunza hapa ili uweze kujua kwa sababu ni muhimu sana kwa wewe kufikia malengo yako. Ni lazima ujue gharama ya muda wako ili usiutumie tu hovyo.

  Sote tunajua kwamba ni lazima kuwa na malengo kwenye maisha na kwamba malengo yamegawanyika kwenye makundi mbalimbali. Kundi mojawapo la malengo ni malengo ya kifedha.

  Ili kuweza kujua gharama ya muda wako kwanza ni lazima uwe na maengo ya kifedha. Kwa mfano kama lengo lako ni kupata shilingi milioni ishirini(tsh 20,000,000/=) ndani ya mwaka mmoja ujao ni rahisi kujua saa yako moja itagharimu shiingi ngapi.

wekundu

Mwaka mmoja una wiki hamsini na mbili(52), tukindoa wiki nne za kupumzika ama likizo zinabaki wiki 48 za kufanya kazi. Wiki moja ina siku tano za kufanya kazi(hiki ni kiwango cha chini kuna wengine wana siku 6 au 7) kwa kutumia siku tano za wiki kwa wiki 48 utakuwa na siku 240 za kufanya kazi kwa mwaka.

  Siku moja ina masaa nane(8) ya kufanya kazi, hichi pia ni kiwango kidogo ila kuna wenye mpaka masaa 12 ya kufanya kazi kwa siku. kwenye siku 240 za kazi kwa mwaka utakuwa na masaa 1920 ya kufanya kazi kwa mwaka.

  Ukigawanya milioni 20 unazotaka kupata kwa mwaka kwa masaa 1920 ya kufanya kazi unapata shilingi 10, 416/=. Kwa hiyo kwa hesabu za karibu ni shilingi  elfu kumi kwa saa.

  Hivyo kama unataka kutengeneza shilingi milioni ishirini(20,000,000/=) kwa mwaka inabidi kila saa (katika masaa nane ya kufanya kazi kwa siku) uitengeneze shilingi elfu kumi(10,000/=).

PESA TZ

Hayo ni mahesabu kwa kiwango hich cha hela ila unaweza kufanya kulingana na kiwango unachotaka wewe inaweza kuwa pungufu ya hapo ama zaidi ya hapo.

  Pia katika hesabu zako ni vyema kutenga muda wa dharura kwa mambo yatakayojitokeza yatakayoweza kusababisha usifanye kazi, kwa mfano magonjwa ama misiba ya watu wa karibu. Sio muda mwingi sana hivyo kama unatumia zaidi ya saa nane kwa siku kufanya kazi(na ni lazima kufanya hivyo kama unataka kuleta tofauti) bado hesabu zitakuwa sawa na hizo.

  Unafanya nini pale ambapo huna kazi ya kufanya?

  Unaweza kuwa umeshafanya hesabu zako na kupata gharama za muda wako. Ila kwa sasa huna kazi unayofanya ili kuingiza kipato hicho kwa saa! Ama unaweza kusema kwa kuwa sasa huna kazi ama biashara unayofanya hivyo huna haja ya kufanya hesabu hizo!

  Hata kama kwa sasa huna kazi unayofanya, ni muhimu kufanya hesabu hizo kwa kuwa tayari una malengo ya kufikia hatua fuani. Baada ya kujua gharama zako basi hakikisha kila saa unaitumia kukuweka kwenye mazingira ya kupata kiasi ulichopanga. Kama gharama ya saa yako moja ni shilingi elfu kumi basi kila unachofanya kikuweke kwenye mazingira ya kuja kutengeneza hiyo elfu kumi ama zaidi. Inaweza kuwa kwa kuendelea kujifunza, ama kutengeneza mtandao wa watu amba ni muhimu kwa ujuzi ulionao.

Posted at Tuesday, July 30, 2013 |  by Makirita Amani

0 comments:

USIACHE KUWEKA MAONI YAKO HAPA.

  Mahafali ya kuhitimu mafunzo ama elimu yoyote ni wakati wa furaha sana kwa wahitimu. Furaha hiyo inatokana na kukamilisha na kupata ujuzi mtu aliokuwa anasomea ama kujifunza. Katika furaha hiyo hiyo kuna wengi wanafurahia kwa sababu ndio wamemaliza kusoma hivyo hawatajisomea tena mpaka labda watakapokuja kuendeea ngazi ya juu ya eimu hiyo. Tumekuwa tukisikia watu wakitoa kauli za kwamba shue imeisha hivyo wanaachana na kusoma na kuanza kufanya mambo yao.

mahafali

  Watanzania hatuna sana mwamko wa kujisomea vitabu mbalimbali. Ndio maana hata shuleni na vyuoni wengi hujisomea kwa sababu tu kuna mtihani na usipojisomea utafeli mtihani na hutofuzu mafunzo yako. Hii ndio inafanya mtu kufurahia kumaliza mafunzo kwa sababu unaona ndio umeachana na vitabu.

  Kama una mpango wa kuachana na vitabu baada ya masomo ama ulishaachana na vitabu ulipomaliza masomo basi jua upo katika njia mbovu ambayo inaelekea kukupoteza. Kwenye ulimwengu wa sasa ambao mambo yanabadiika kwa kasi ni rahisi sana kuachwa nyuma kama hakuna kipya unachoingiza kwenye kichwa chako kia siku. Hizi ni zama za taarifa ambapo wenye taarifa sahihi ndio wanaotawala.

  Ili kupata taarifa na kungeza ufahamu wako ni vyema ukapenda kujisomea. Weka utaratibu wa kujisomea vitabu ambavyo vinahusiana na kile unachofanya ama kile unachopendelea. Kwa kujisomea vitabu utapata maarifa na mbinu mbalimbali zitakazokufanya uwe na ujuzi zaidi na uwe umebobea kwenye hicho unachofanya.

kujisomeakusoma2

  Sina muda wa kujismea kila siku, niko ‘bize’ sana.

  Unaweza ukawa umeshaelewa umuhimu wa kujisomea ila tatizo lako ni moja tu, huna muda. Ni kwei kabisa unaweza kuwa huna muda kutokana na mihangaiko ya sasa na ugumu wa maisha, lakini hupaswi kukosa muda mfupi wa kujisomea kila siku. Tenga japo nusu saa tu kwa siku ya kujisomea, hakuna unaloweza kupoteza kwa kutenga nusu sasa(tena kwa kuwahi kuamka asubuhi) kila siku. Bonyeza hapa kwa kupata mpango mzuri wa muda wa kujisomea.

  Sina vitabu vya kujisomea.

vitabu

  Inawezekana unapenda sana kujisomea ama umeshaona umuhimu wa kujisomea, na umeshaweka ratiba nzuri ya kujisomea kila siku ila huna vitabu vya kujisomea. Kwa uimwengu wa sasa vitabu vinapatikana kiurahisi mno, licha ya vitabu pia kuna mitandao mingi inayotoa taarifa nzuri za wewe kuweza kujiendeleza. Kama unataka kitabu chochote cha kada yoyote unayofanya ama unayopendelea unaweza kuwasiliana na mimi na nikakupatia kitabu unachotaka bila gharama yoyote. Bonyeza hapa na utapata mawasiiano yangu ya email au namba ya simu.

  Kama hujawa na utaratibu wa kujisomea vitabu mpaka sasa hujachelewa kama utaamua kuchukua hatua leo. Jiwekee ratiba ya kusoma vitabu na ndani ya muda mfupi utaanza kuona matunda yake kwa lolote unalofanya.

UMESOMA VITABU VINGAPI?

  Mahafali ya kuhitimu mafunzo ama elimu yoyote ni wakati wa furaha sana kwa wahitimu. Furaha hiyo inatokana na kukamilisha na kupata ujuzi mtu aliokuwa anasomea ama kujifunza. Katika furaha hiyo hiyo kuna wengi wanafurahia kwa sababu ndio wamemaliza kusoma hivyo hawatajisomea tena mpaka labda watakapokuja kuendeea ngazi ya juu ya eimu hiyo. Tumekuwa tukisikia watu wakitoa kauli za kwamba shue imeisha hivyo wanaachana na kusoma na kuanza kufanya mambo yao.

mahafali

  Watanzania hatuna sana mwamko wa kujisomea vitabu mbalimbali. Ndio maana hata shuleni na vyuoni wengi hujisomea kwa sababu tu kuna mtihani na usipojisomea utafeli mtihani na hutofuzu mafunzo yako. Hii ndio inafanya mtu kufurahia kumaliza mafunzo kwa sababu unaona ndio umeachana na vitabu.

  Kama una mpango wa kuachana na vitabu baada ya masomo ama ulishaachana na vitabu ulipomaliza masomo basi jua upo katika njia mbovu ambayo inaelekea kukupoteza. Kwenye ulimwengu wa sasa ambao mambo yanabadiika kwa kasi ni rahisi sana kuachwa nyuma kama hakuna kipya unachoingiza kwenye kichwa chako kia siku. Hizi ni zama za taarifa ambapo wenye taarifa sahihi ndio wanaotawala.

  Ili kupata taarifa na kungeza ufahamu wako ni vyema ukapenda kujisomea. Weka utaratibu wa kujisomea vitabu ambavyo vinahusiana na kile unachofanya ama kile unachopendelea. Kwa kujisomea vitabu utapata maarifa na mbinu mbalimbali zitakazokufanya uwe na ujuzi zaidi na uwe umebobea kwenye hicho unachofanya.

kujisomeakusoma2

  Sina muda wa kujismea kila siku, niko ‘bize’ sana.

  Unaweza ukawa umeshaelewa umuhimu wa kujisomea ila tatizo lako ni moja tu, huna muda. Ni kwei kabisa unaweza kuwa huna muda kutokana na mihangaiko ya sasa na ugumu wa maisha, lakini hupaswi kukosa muda mfupi wa kujisomea kila siku. Tenga japo nusu saa tu kwa siku ya kujisomea, hakuna unaloweza kupoteza kwa kutenga nusu sasa(tena kwa kuwahi kuamka asubuhi) kila siku. Bonyeza hapa kwa kupata mpango mzuri wa muda wa kujisomea.

  Sina vitabu vya kujisomea.

vitabu

  Inawezekana unapenda sana kujisomea ama umeshaona umuhimu wa kujisomea, na umeshaweka ratiba nzuri ya kujisomea kila siku ila huna vitabu vya kujisomea. Kwa uimwengu wa sasa vitabu vinapatikana kiurahisi mno, licha ya vitabu pia kuna mitandao mingi inayotoa taarifa nzuri za wewe kuweza kujiendeleza. Kama unataka kitabu chochote cha kada yoyote unayofanya ama unayopendelea unaweza kuwasiliana na mimi na nikakupatia kitabu unachotaka bila gharama yoyote. Bonyeza hapa na utapata mawasiiano yangu ya email au namba ya simu.

  Kama hujawa na utaratibu wa kujisomea vitabu mpaka sasa hujachelewa kama utaamua kuchukua hatua leo. Jiwekee ratiba ya kusoma vitabu na ndani ya muda mfupi utaanza kuona matunda yake kwa lolote unalofanya.

Posted at Tuesday, July 30, 2013 |  by Makirita Amani

0 comments:

USIACHE KUWEKA MAONI YAKO HAPA.

Monday, July 29, 2013

  Web programming au programming za aina nyingine ni ujuzi ambao unaweza kujifunza bila kuwa na 'background' ya sayansi. Kinachotakiwa ni Kupenda (interest) na pia kujituma kukariri na kufanya mazoezi ya kutumia 'codes'.
Nakualika wewe ambaye una interest ya kujifunza programming, uanze kujifunza HTML kwani ndio programming language mama katika web site development.
  Na ili uive vema katika kuunda website, Somo hili la kwanza litahusu kukupa ufahamu jinsi Website zinavyofanya kazi, jinsi ambavyo utaweza kuanza kutengeneza website yako ya kwanza. Fuatilia kwa umakini maelezo yote, na Jitahidi Ujibu maswali mwisho wa somo bila 'kugezea'.

KWA KUSOMA KOZI HII INGIA HAPA

JIFUNZE WEBSITE PROGRAMMING; SOMO LA KWANZA

http://mbuke.blogspot.com/2013/07/jifunze-website-programming-somo-la-1.html

JIFUNZE WEBSITE PROGRAMMING

  Web programming au programming za aina nyingine ni ujuzi ambao unaweza kujifunza bila kuwa na 'background' ya sayansi. Kinachotakiwa ni Kupenda (interest) na pia kujituma kukariri na kufanya mazoezi ya kutumia 'codes'.
Nakualika wewe ambaye una interest ya kujifunza programming, uanze kujifunza HTML kwani ndio programming language mama katika web site development.
  Na ili uive vema katika kuunda website, Somo hili la kwanza litahusu kukupa ufahamu jinsi Website zinavyofanya kazi, jinsi ambavyo utaweza kuanza kutengeneza website yako ya kwanza. Fuatilia kwa umakini maelezo yote, na Jitahidi Ujibu maswali mwisho wa somo bila 'kugezea'.

KWA KUSOMA KOZI HII INGIA HAPA

JIFUNZE WEBSITE PROGRAMMING; SOMO LA KWANZA

http://mbuke.blogspot.com/2013/07/jifunze-website-programming-somo-la-1.html

Posted at Monday, July 29, 2013 |  by Makirita Amani

0 comments:

USIACHE KUWEKA MAONI YAKO HAPA.

  Kwenye mtandao wa facebook kuna matapeli huwa wanawatumia watu ujumbe wa kutaka urafiki nao. Mara nyingi matapeli hao huweka picha ya mwanamke mrembo na hutuma ujumbe kwamba wamevutiwa na wewe na wanataka muwe wapenzi. Nadhani umewahi kupata ujumbe kama huo, mimi kila siku napata jumbe hizo na nimeshazizoea na huwa sihangaiki kuzifuatilia.

  Matapeli wa aina hii inasemekana wengi wanatokea Nigeria na jumbe zao nyingi wanazituma kwa lugha ya kiingereza.

scamscam2

  Juzi nimepata tena ujumbe huo ila huu ulinistua kidogo, tofauti na niivyozoea kupata ujumbe ulioandikwa kwa lugha ya kiingereza, huo niliopata uitafsiriwa kwa kiswahii pia.

Conversation started Saturday
11:49pm
Marbel Johnson
hujambo wapenzi i am miss ya Marbel Johnson i ni nzuri sana kuangalia vijana, kutafuta kwa ajili ya upendo wa kweli Serious na nzuri sana na ya kueleweka mtu vijana kwamba anajua maana ya kweli ya upendo. Nilikwenda kwa maelezo yako na i kusoma na kuchukua riba ndani yake, tafadhali kama huna akili i mapenzi kama wewe kuandika mimi kwenye ID hii tafadhali hii ni anwani yangu ya barua pepe (marbeljohnson_o@ymail.com) Naamini umbali na umri haijalishi katika uhusiano mbaya lakini upendo mambo zaidi. matumaini ya kusikia kutoka kwenu hivi karibuni, na i na muhimu sana ya kujadili suala hilo na wewe. yako Marbel
°°°°°°°°°°°°°°°°°°° hello dear i am miss marbel johnson i am very good looking young, seeking for Serious true love with a very good and understandable young someone that knows the true meaning of love. I went through your profile and i read it and took interest in it, please if you don't mind i will like you to write me on this ID please this is my email address ( marbeljohnson_o@ymail.com) I believe distance and age doesn't matter in a serious relationship but love matters most . hoping to hear from you soon,and i have very important issue to discuss with you . yours marbel

  Hii iinifanya nifikiri kwa muda, kwa nini wameamua kutafsiri? Nikapata wazo kwamba baada ya kuona sijibu wameona wabadili mbinu za kunifikia huenda walihisi sielewi kiingereza hivyo wakabadili na kutumia kiswahili.

  Kama mpaka matapeli ni wabunifu inakuwaje wewe unashindwa kuwa mbunifu? Ubunifu ndio njia pekee ya kukutofautisha wewe na wengine na ndio njia nzuri itakayokufanya uweze kufikia ndoto na malengo yako bila matatizo.

  Kwa lolote unalofanya hakikisha unatumia ubunifu wa kipekee ili uweze kupata matokeo bora. Kila mtu ni mbunifu ni wewe tu kuamua kuanza kutumia ubunifu wako. 

MAISHA YANAVYOZIDI KUWA MAGUMU MATAPELI NAO WANAONGEZA UBUNIFU.

  Kwenye mtandao wa facebook kuna matapeli huwa wanawatumia watu ujumbe wa kutaka urafiki nao. Mara nyingi matapeli hao huweka picha ya mwanamke mrembo na hutuma ujumbe kwamba wamevutiwa na wewe na wanataka muwe wapenzi. Nadhani umewahi kupata ujumbe kama huo, mimi kila siku napata jumbe hizo na nimeshazizoea na huwa sihangaiki kuzifuatilia.

  Matapeli wa aina hii inasemekana wengi wanatokea Nigeria na jumbe zao nyingi wanazituma kwa lugha ya kiingereza.

scamscam2

  Juzi nimepata tena ujumbe huo ila huu ulinistua kidogo, tofauti na niivyozoea kupata ujumbe ulioandikwa kwa lugha ya kiingereza, huo niliopata uitafsiriwa kwa kiswahii pia.

Conversation started Saturday
11:49pm
Marbel Johnson
hujambo wapenzi i am miss ya Marbel Johnson i ni nzuri sana kuangalia vijana, kutafuta kwa ajili ya upendo wa kweli Serious na nzuri sana na ya kueleweka mtu vijana kwamba anajua maana ya kweli ya upendo. Nilikwenda kwa maelezo yako na i kusoma na kuchukua riba ndani yake, tafadhali kama huna akili i mapenzi kama wewe kuandika mimi kwenye ID hii tafadhali hii ni anwani yangu ya barua pepe (marbeljohnson_o@ymail.com) Naamini umbali na umri haijalishi katika uhusiano mbaya lakini upendo mambo zaidi. matumaini ya kusikia kutoka kwenu hivi karibuni, na i na muhimu sana ya kujadili suala hilo na wewe. yako Marbel
°°°°°°°°°°°°°°°°°°° hello dear i am miss marbel johnson i am very good looking young, seeking for Serious true love with a very good and understandable young someone that knows the true meaning of love. I went through your profile and i read it and took interest in it, please if you don't mind i will like you to write me on this ID please this is my email address ( marbeljohnson_o@ymail.com) I believe distance and age doesn't matter in a serious relationship but love matters most . hoping to hear from you soon,and i have very important issue to discuss with you . yours marbel

  Hii iinifanya nifikiri kwa muda, kwa nini wameamua kutafsiri? Nikapata wazo kwamba baada ya kuona sijibu wameona wabadili mbinu za kunifikia huenda walihisi sielewi kiingereza hivyo wakabadili na kutumia kiswahili.

  Kama mpaka matapeli ni wabunifu inakuwaje wewe unashindwa kuwa mbunifu? Ubunifu ndio njia pekee ya kukutofautisha wewe na wengine na ndio njia nzuri itakayokufanya uweze kufikia ndoto na malengo yako bila matatizo.

  Kwa lolote unalofanya hakikisha unatumia ubunifu wa kipekee ili uweze kupata matokeo bora. Kila mtu ni mbunifu ni wewe tu kuamua kuanza kutumia ubunifu wako. 

Posted at Monday, July 29, 2013 |  by Makirita Amani

0 comments:

USIACHE KUWEKA MAONI YAKO HAPA.

  Umepanda meli na humo kwenye meli mpo watu wengi baadhi ni abiria tu wanaosafirishwa na wengine ni sehemu ya mabaharia wanaohakikisha meli inafika inakoelekea. Ghafla hali ya bahari inabadilika na meli inayumba sana na ili kuweza kuendelea na safari inabidi baadhi ya watu watoswe majini ili kupunguza uzito. Unafikiri ni watu gani watakaotoswa majini? Abiria ama baharia?

MELIMELI2

  Sote tunakubali kwamba watakaotoswa majini ni abiria. Hakuna anaeweza hata kufikiria kwamba baharia atoswe majini. Kwa nini baharia asitoswe na abiria wengine waweze kutoswa? Wote si ni binadamu sawa? Katika hali kama hiyo kinachojalisha sio ubinadamu bali umuhimu. Baharia anaachwa kwa sababu yeye ni wa muhimu kwenye chombo kuliko abiria wa kawaida.

  Jiulize wewe je kwenye meli uliyopanda wewe ni abiria wa kawaida ama sehemu ya mabaharia?

  Kwenye maisha yako kuna meli nyingi ulizopanda, baadhi ya meli hizo ni ajira, na nafasi mbali mbali kwenye jamii.

  Kwa mfano kwenye ajira kama kampuni ama shirika unalofanya kazi likipata msukosuko na kuhitaji kupunguza wafanyakazi watakaoanza kupunguzwa ni wale ambao hawana umuhimu mkubwa kwa shirika. Yaani watapunguzwa wale ambao ni mzigo, ambao hata wasipokuwepo hakuwezi kuwa na athari kubwa sana.

FIREDFIRED2

  Jitafakari kwenye ajira yako wewe ni baharia ama abiria? Je kuna kipi cha muhimu sana ambacho kampuni ama shirika linapata kutoka kwako. Je ni rahisi tu kwa wewe kupunguzwa ama kufukuzwa?

  Sio lazima uwe mkurugenzi ama injinia mkuu ndio uwe wa muhimu sana kwenye sehemu yako ya kazi. Hata kama wewe ni mfanya usafi tu unaweza kuamua kuwa wa muhimu sana kiasi kwamba sio rahisi kwa wewe kuondolewa. Kwa sababu hata wapunguzwe wafanyakazi kwa asilimia 70 bado lazima atabakishwa mfanya usafi japo mmoja. Unafikiri kitatumika kigezo gani kumbakisha huyo mmoja?

  Kwenye kitengo chochote unachofanya kazi unaweza kuwa wa muhimu sana na kufanya iwe ngumu kuondolewa kirahisi.

  Ili uwe wa muhimu ni lazima kile unachofanya ufanye kwa utofauti na kwa kiwango cha hali ya juu. Ni rahisi kwako kuweza kufanya hivyo kama utatumia uwezo na vipaji vya pekee ulivyonavyo.

  Hakikisha chochote unachofanya unaleta mabadiliko kwako na kwa wanaokuzunguka. Mabadiliko hayo yatakufanya uwe wa pekee na kuwa wa muhimu kwenye kazi unayofanya.

 

JE WEWE NI BAHARIA AMA ABIRIA?

  Umepanda meli na humo kwenye meli mpo watu wengi baadhi ni abiria tu wanaosafirishwa na wengine ni sehemu ya mabaharia wanaohakikisha meli inafika inakoelekea. Ghafla hali ya bahari inabadilika na meli inayumba sana na ili kuweza kuendelea na safari inabidi baadhi ya watu watoswe majini ili kupunguza uzito. Unafikiri ni watu gani watakaotoswa majini? Abiria ama baharia?

MELIMELI2

  Sote tunakubali kwamba watakaotoswa majini ni abiria. Hakuna anaeweza hata kufikiria kwamba baharia atoswe majini. Kwa nini baharia asitoswe na abiria wengine waweze kutoswa? Wote si ni binadamu sawa? Katika hali kama hiyo kinachojalisha sio ubinadamu bali umuhimu. Baharia anaachwa kwa sababu yeye ni wa muhimu kwenye chombo kuliko abiria wa kawaida.

  Jiulize wewe je kwenye meli uliyopanda wewe ni abiria wa kawaida ama sehemu ya mabaharia?

  Kwenye maisha yako kuna meli nyingi ulizopanda, baadhi ya meli hizo ni ajira, na nafasi mbali mbali kwenye jamii.

  Kwa mfano kwenye ajira kama kampuni ama shirika unalofanya kazi likipata msukosuko na kuhitaji kupunguza wafanyakazi watakaoanza kupunguzwa ni wale ambao hawana umuhimu mkubwa kwa shirika. Yaani watapunguzwa wale ambao ni mzigo, ambao hata wasipokuwepo hakuwezi kuwa na athari kubwa sana.

FIREDFIRED2

  Jitafakari kwenye ajira yako wewe ni baharia ama abiria? Je kuna kipi cha muhimu sana ambacho kampuni ama shirika linapata kutoka kwako. Je ni rahisi tu kwa wewe kupunguzwa ama kufukuzwa?

  Sio lazima uwe mkurugenzi ama injinia mkuu ndio uwe wa muhimu sana kwenye sehemu yako ya kazi. Hata kama wewe ni mfanya usafi tu unaweza kuamua kuwa wa muhimu sana kiasi kwamba sio rahisi kwa wewe kuondolewa. Kwa sababu hata wapunguzwe wafanyakazi kwa asilimia 70 bado lazima atabakishwa mfanya usafi japo mmoja. Unafikiri kitatumika kigezo gani kumbakisha huyo mmoja?

  Kwenye kitengo chochote unachofanya kazi unaweza kuwa wa muhimu sana na kufanya iwe ngumu kuondolewa kirahisi.

  Ili uwe wa muhimu ni lazima kile unachofanya ufanye kwa utofauti na kwa kiwango cha hali ya juu. Ni rahisi kwako kuweza kufanya hivyo kama utatumia uwezo na vipaji vya pekee ulivyonavyo.

  Hakikisha chochote unachofanya unaleta mabadiliko kwako na kwa wanaokuzunguka. Mabadiliko hayo yatakufanya uwe wa pekee na kuwa wa muhimu kwenye kazi unayofanya.

 

Posted at Monday, July 29, 2013 |  by Makirita Amani

0 comments:

USIACHE KUWEKA MAONI YAKO HAPA.

Sunday, July 28, 2013

  Tofauti kubwa kati ya binadamu na viumbe wengine ni uwezo mkubwa tuliopewa binadamu wa kuweza kubadili mazingira yanayotuzunguka. Binadamu tunauwezo mkubwa wa kugundua vitu vya aina mbalimbali. Pamoja na kuwa na uwezo huo mkubwa wa kugundua mambo bado sio wote wanaogundua vitu vipya. Kuna tofauti gani kati ya wagunduzi na watu wengine?

  Kabla ya kitu chochote kugunduliwa ni lazima mgunduzi aone matokeo ya kitu anachotaka kufanya kabla hata hajaanza kukifanya. Ni lazima mgunduzi aone picha kamili ya matokeo ya kile anachofanya. Picha hiyo ndio inampa nguvu na hamu kubwa ya kufanya ili kufikia picha hiyo. Kuweza kuiona picha isiyokuwepo ndio tofauti kubwa ya wanaofanikiwa na wanaoshindwa ama wagunduzi na watu wengine.

                              ndoto

  Picha hiyo inapatikana vipi? Picha hiyo inapatikana kwa kuwa na ndoto. Ndoto tunayozungumzia hapa sio ya kulala na kuota usiku, hapana, hii ni hali ya kuona mbele na kuwa na kiu ya kufanya jambo ili kufikia kule unakoona. Ndoto ndiyo inayotengeneza picha kubwa ya mambo yatakavyobadilika kwa wewe kufanya kile unachohitajika kufanya.

  Bila ya kuwa na ndoto ni vigumu sana kufanya mabadiliko kwenye maisha yako na maisha ya wanaokuzunguka. Ndoto ndiyo inayokufanya kutengeneza malengo ya maisha yako na mipango ya kuitekeleza.

  Kwa nini wengi hawaleti mabadiliko? Watu wengi wanapita duniani bila ya kuleta mabadiliko yoyote hata kwa wao binafsi kwa sababu wanaamua kutokuwa na ndoto. Japokuwa hakuna gharama yoyote kuwa na ndoto lakini wengi hawataki tu kuota. Wewe ndoto yako ni nini?

  Huwezi kufanikiwa maishani kwa kufanya tu kila linalokuja mbele yako, lazima uwe na ndoto kisha uweke malengo na mipango ya kufikia ndoto hiyo. Lazima ujue unakokwenda ili ujue jinsi ya kufika huko.

  Ota ndoto yako na iwe ndoto kubwa ambayo kila siku inakupa nguvu ya kufanya kazi kwa bidii ili uweze kuifikia. 

UNA NDOTO?

  Tofauti kubwa kati ya binadamu na viumbe wengine ni uwezo mkubwa tuliopewa binadamu wa kuweza kubadili mazingira yanayotuzunguka. Binadamu tunauwezo mkubwa wa kugundua vitu vya aina mbalimbali. Pamoja na kuwa na uwezo huo mkubwa wa kugundua mambo bado sio wote wanaogundua vitu vipya. Kuna tofauti gani kati ya wagunduzi na watu wengine?

  Kabla ya kitu chochote kugunduliwa ni lazima mgunduzi aone matokeo ya kitu anachotaka kufanya kabla hata hajaanza kukifanya. Ni lazima mgunduzi aone picha kamili ya matokeo ya kile anachofanya. Picha hiyo ndio inampa nguvu na hamu kubwa ya kufanya ili kufikia picha hiyo. Kuweza kuiona picha isiyokuwepo ndio tofauti kubwa ya wanaofanikiwa na wanaoshindwa ama wagunduzi na watu wengine.

                              ndoto

  Picha hiyo inapatikana vipi? Picha hiyo inapatikana kwa kuwa na ndoto. Ndoto tunayozungumzia hapa sio ya kulala na kuota usiku, hapana, hii ni hali ya kuona mbele na kuwa na kiu ya kufanya jambo ili kufikia kule unakoona. Ndoto ndiyo inayotengeneza picha kubwa ya mambo yatakavyobadilika kwa wewe kufanya kile unachohitajika kufanya.

  Bila ya kuwa na ndoto ni vigumu sana kufanya mabadiliko kwenye maisha yako na maisha ya wanaokuzunguka. Ndoto ndiyo inayokufanya kutengeneza malengo ya maisha yako na mipango ya kuitekeleza.

  Kwa nini wengi hawaleti mabadiliko? Watu wengi wanapita duniani bila ya kuleta mabadiliko yoyote hata kwa wao binafsi kwa sababu wanaamua kutokuwa na ndoto. Japokuwa hakuna gharama yoyote kuwa na ndoto lakini wengi hawataki tu kuota. Wewe ndoto yako ni nini?

  Huwezi kufanikiwa maishani kwa kufanya tu kila linalokuja mbele yako, lazima uwe na ndoto kisha uweke malengo na mipango ya kufikia ndoto hiyo. Lazima ujue unakokwenda ili ujue jinsi ya kufika huko.

  Ota ndoto yako na iwe ndoto kubwa ambayo kila siku inakupa nguvu ya kufanya kazi kwa bidii ili uweze kuifikia. 

Posted at Sunday, July 28, 2013 |  by Makirita Amani

0 comments:

USIACHE KUWEKA MAONI YAKO HAPA.

Friday, July 26, 2013

  Wengi tunajua michezo ya bahati nasibu na wengi wetu tumewahi kucheza michezo hiyo. Kwa hapa tanzania iikuwepo michezo mikubwa ya bahati nasibu kama jackpot bingo, lotto kitita na mingineyo. Kwa sasa michezo hii inachezeshwa sana na makampuni mbalimbali kuongeza mauzo ya bidhaa zao. Makampuni ya simu na vileo ndio kwa sasa yanaendesha michezo mingi ya aina hii.

bahati

  Kwenye bahati nasibu yoyote huwa wanashiriki watu wengi sana. Ila mshindi huishia kuwa mmoja ama watatu waliobahatika. Wengine hakuna atakaefahamu kama hata walishiriki bahati nasibu hiyo. Kuna uwezekano umeshiriki bahati nasibu nyingi sana, ila kama hujawahi kuwa kati ya wachache waliobahatika kushinda basi hakuna anaejua kama hata ulishiriki.

bahati2

  Jamii inayotuzunguka haina tofauti na mfumo wa bahati nasibu. Unaweza kuwa unafanya jambo zuri ila kama halionekani ama halijaigusa jamii basi hakuna atakaejua kama unafanya jambo lolote.

  Usikate tamaa kama hakuna anaekuona sasa hivi, endelea na mipango yako na mwisho wa siku itadhihirika kwa kila mtu.

  Hakuna mtu aliefanya mabadiliko na yakaanza kunekana mara moja, mabadiliko mengi huchukua muda kueleweka hivyo usikate tamaa.

  Hakikisha unaleta mabadiliko kwenye kile unachofanya iwe biashara ama ajira. Yafanye maisha ya binadamu yawe rahisi na yakufurahia. Usikate tamaa kama hakuna anaekuelewa kwa sasa, ndivyo jamii ilivyo.

SOMO TUNALOWEZA KUJIFUNZA KUTOKA KWENYE BAHATI NASIBU

  Wengi tunajua michezo ya bahati nasibu na wengi wetu tumewahi kucheza michezo hiyo. Kwa hapa tanzania iikuwepo michezo mikubwa ya bahati nasibu kama jackpot bingo, lotto kitita na mingineyo. Kwa sasa michezo hii inachezeshwa sana na makampuni mbalimbali kuongeza mauzo ya bidhaa zao. Makampuni ya simu na vileo ndio kwa sasa yanaendesha michezo mingi ya aina hii.

bahati

  Kwenye bahati nasibu yoyote huwa wanashiriki watu wengi sana. Ila mshindi huishia kuwa mmoja ama watatu waliobahatika. Wengine hakuna atakaefahamu kama hata walishiriki bahati nasibu hiyo. Kuna uwezekano umeshiriki bahati nasibu nyingi sana, ila kama hujawahi kuwa kati ya wachache waliobahatika kushinda basi hakuna anaejua kama hata ulishiriki.

bahati2

  Jamii inayotuzunguka haina tofauti na mfumo wa bahati nasibu. Unaweza kuwa unafanya jambo zuri ila kama halionekani ama halijaigusa jamii basi hakuna atakaejua kama unafanya jambo lolote.

  Usikate tamaa kama hakuna anaekuona sasa hivi, endelea na mipango yako na mwisho wa siku itadhihirika kwa kila mtu.

  Hakuna mtu aliefanya mabadiliko na yakaanza kunekana mara moja, mabadiliko mengi huchukua muda kueleweka hivyo usikate tamaa.

  Hakikisha unaleta mabadiliko kwenye kile unachofanya iwe biashara ama ajira. Yafanye maisha ya binadamu yawe rahisi na yakufurahia. Usikate tamaa kama hakuna anaekuelewa kwa sasa, ndivyo jamii ilivyo.

Posted at Friday, July 26, 2013 |  by Makirita Amani

0 comments:

USIACHE KUWEKA MAONI YAKO HAPA.

  Waswahili wanasema ‘nyota njema huonekana asubuhi’, hawakuishia hapo, wanasema pia ‘biashara asubuhi, jioni mahesabu’. Kwenye semi hizo inaonesha kabisa kwamba mambo yote yanategemea mwanzo ukoje. Yaani jibu la mwisho inategemea na umeanzaje.

new daynew day2

  Hivyo ndivyo ilivyo kwa siku pia, siku inayokwenda vizuri na kuisha vizuri ni siku iliyanzwa vizuri. Usitegemee kuanza siku yako kwa kisirani halafu iishe kwa furaha, ni ngumu sana.

  Ianze siku yako kwa mambo makuu mawili, kwanza furahia na shukuru kwa kuianza siku na pili tegemea kufanya makubwa kwenye siku yako.

  Shukuru kwa kuiona siku mpya na furahia kwa kuwa ni siku pekee unayoweza kufanya kile ulichopanga kufanya. Hakikisha hakuna ‘anaekuvuruga’ na kundoa furaha yako asubuhi na mapema. Jitahidi kufurahia siku yako asubuhi ili siku nzima ujawe na furaha.

  Tegemea kufanya makubwa kwenye siku yako. Tayari umepanga siku yako kabla ya kulala, na leo umeamka ukiwa na furaha tayari kwa kwenda kutekeleza mipango yako. Tegemea matokeo mazuri na makubwa kutoka kwenye mipango yako. Tegemea kufanya mabadiliko na kusaidia watu.

  Hakikisha uso wako umevaa tabasamu siku nzima, ndio, tabasamu kwa sababu umeamua kuyafurahia maisha. Usikubali tabasamu lako liondolewe na mtu ama kitu chochote. Kama kuna kitu ama mtu anakuharibia tabasamu lako basi ni bora kutafuta njia ya kubadili hiyo hali.

smilesmile2

  Siku hii ni yako na wewe mwenyewe ndiye unaeweza kuchagua jinsi unavyotaka iende. Amua kuwa na siku nzuri iliyojaa furaha na uzalishaji. Anza siku yako vyema na uyafurahie maisha.

IANZE SIKU YAKO HIVI….

  Waswahili wanasema ‘nyota njema huonekana asubuhi’, hawakuishia hapo, wanasema pia ‘biashara asubuhi, jioni mahesabu’. Kwenye semi hizo inaonesha kabisa kwamba mambo yote yanategemea mwanzo ukoje. Yaani jibu la mwisho inategemea na umeanzaje.

new daynew day2

  Hivyo ndivyo ilivyo kwa siku pia, siku inayokwenda vizuri na kuisha vizuri ni siku iliyanzwa vizuri. Usitegemee kuanza siku yako kwa kisirani halafu iishe kwa furaha, ni ngumu sana.

  Ianze siku yako kwa mambo makuu mawili, kwanza furahia na shukuru kwa kuianza siku na pili tegemea kufanya makubwa kwenye siku yako.

  Shukuru kwa kuiona siku mpya na furahia kwa kuwa ni siku pekee unayoweza kufanya kile ulichopanga kufanya. Hakikisha hakuna ‘anaekuvuruga’ na kundoa furaha yako asubuhi na mapema. Jitahidi kufurahia siku yako asubuhi ili siku nzima ujawe na furaha.

  Tegemea kufanya makubwa kwenye siku yako. Tayari umepanga siku yako kabla ya kulala, na leo umeamka ukiwa na furaha tayari kwa kwenda kutekeleza mipango yako. Tegemea matokeo mazuri na makubwa kutoka kwenye mipango yako. Tegemea kufanya mabadiliko na kusaidia watu.

  Hakikisha uso wako umevaa tabasamu siku nzima, ndio, tabasamu kwa sababu umeamua kuyafurahia maisha. Usikubali tabasamu lako liondolewe na mtu ama kitu chochote. Kama kuna kitu ama mtu anakuharibia tabasamu lako basi ni bora kutafuta njia ya kubadili hiyo hali.

smilesmile2

  Siku hii ni yako na wewe mwenyewe ndiye unaeweza kuchagua jinsi unavyotaka iende. Amua kuwa na siku nzuri iliyojaa furaha na uzalishaji. Anza siku yako vyema na uyafurahie maisha.

Posted at Friday, July 26, 2013 |  by Makirita Amani

0 comments:

USIACHE KUWEKA MAONI YAKO HAPA.

  Kutokana na mihangaiko ya kila siku kuna badhi ya watu wanajikuta hawana ratiba ama utaratibu wa kupata kifungua kinywa. Wengine wanaacha kupata kifungua kinywa makusudi kwa lengo la kupunguza uzito na kuna wengine wanakosa kifungua kinywa kwa sababu za kifedha.

breakfastbreakfast2

  Inawezekana pia kutokana na shughuli zako nyingi ama ratiba zako unachelewa sana kupata kifungua kinywa.

  Bila ya kujali ni sababu gani inayoufanya usipate ama uchelewe kupata kifungua kinywa kuna matatizo ya kiafya yanaweza kukupata kwa kutopata kifungua kinywa.

  Utafiti iliofanywa nchini marekani unaonesha kwamba kutopata kifungua kinywa kunaweza kusababisha shinikizo la damu, kuongezeka uzito, na kungezeka kwa mafuta kwenye damu.

heartunene

  Utafiti huo ulihusisha wanaume 27,000 wenye miaka kati ya 45-82 na ulifanyika kwa miaka 16. Utafiti ulihusisha mitindo ya maisha kama kutokupata kifungua kinywa na magonjwa ya moyo.

  Majibu yananesha kwamba wanaume wasiopata kifungua kinywa wana uwezekano mkubwa zaidi wa kupata magonjwa ya moyo kwa asilimia 27.

  Watafiti hao wanasema chanzo cha magonjwa ya moyo kutokana na kukosa kifungua kinywa  ni mfungo wa muda mrefu unaosababisha mwili kushindwa kufanya kazi vizuri. Tunapolala usiku tunakuwa tumefunga(hatuli usingizini) kama unapoamka huli chochote ina maana unaendeleza mfungo kitu ambacho kinauchosha mwili na kushindwa kuunguza mafuta yaliyopo kwenye damu. Kutokuvunjwa kwa mafuta hayo ndio chanzo cha magonjwa ya moyo na kuongezeka uzito/unene.

  Tatizo hilo la mwili kuchoka pia linatkea pale mtu anapochelewa kupata kifungua kinywa, hivyo inashauriwa kifungua kinywa kipatikane mapema asubuhi ili mwili uweze kufanya kazi zake vizuri.

 

KUTOPATA KIFUNGUAKINYWA NI HATARI KWA AFYA YAKO.

  Kutokana na mihangaiko ya kila siku kuna badhi ya watu wanajikuta hawana ratiba ama utaratibu wa kupata kifungua kinywa. Wengine wanaacha kupata kifungua kinywa makusudi kwa lengo la kupunguza uzito na kuna wengine wanakosa kifungua kinywa kwa sababu za kifedha.

breakfastbreakfast2

  Inawezekana pia kutokana na shughuli zako nyingi ama ratiba zako unachelewa sana kupata kifungua kinywa.

  Bila ya kujali ni sababu gani inayoufanya usipate ama uchelewe kupata kifungua kinywa kuna matatizo ya kiafya yanaweza kukupata kwa kutopata kifungua kinywa.

  Utafiti iliofanywa nchini marekani unaonesha kwamba kutopata kifungua kinywa kunaweza kusababisha shinikizo la damu, kuongezeka uzito, na kungezeka kwa mafuta kwenye damu.

heartunene

  Utafiti huo ulihusisha wanaume 27,000 wenye miaka kati ya 45-82 na ulifanyika kwa miaka 16. Utafiti ulihusisha mitindo ya maisha kama kutokupata kifungua kinywa na magonjwa ya moyo.

  Majibu yananesha kwamba wanaume wasiopata kifungua kinywa wana uwezekano mkubwa zaidi wa kupata magonjwa ya moyo kwa asilimia 27.

  Watafiti hao wanasema chanzo cha magonjwa ya moyo kutokana na kukosa kifungua kinywa  ni mfungo wa muda mrefu unaosababisha mwili kushindwa kufanya kazi vizuri. Tunapolala usiku tunakuwa tumefunga(hatuli usingizini) kama unapoamka huli chochote ina maana unaendeleza mfungo kitu ambacho kinauchosha mwili na kushindwa kuunguza mafuta yaliyopo kwenye damu. Kutokuvunjwa kwa mafuta hayo ndio chanzo cha magonjwa ya moyo na kuongezeka uzito/unene.

  Tatizo hilo la mwili kuchoka pia linatkea pale mtu anapochelewa kupata kifungua kinywa, hivyo inashauriwa kifungua kinywa kipatikane mapema asubuhi ili mwili uweze kufanya kazi zake vizuri.

 

Posted at Friday, July 26, 2013 |  by Makirita Amani

0 comments:

USIACHE KUWEKA MAONI YAKO HAPA.

Thursday, July 25, 2013

  Ukiangalia matatizo uliyonayo, na malengo yako kwenye maisha jibu rahisi unalopata ni ukipata kiasi fulani cha fedha baasi, matatizo bai bai. Au unafikiri ukiweza kulipwa ama kutengeneza kiasi fulani kwa mwezi matatizo kwako ndio mwiko!!

pesa

  Kabla hujajiridhisha na jibu kwamba matatizo yote yanatokana na kukosa fedha fikiria hivi kwanza. Umewahi kugundua kwamba watu wengi huwa wanaishiwa fedha sawa licha ya kuwa na vipato tofauti? Kwa mfano wafanyakazi wengi kila inapokaribia mwisho wa mwezi(kuanzia tarehe ishirini na) wanakuwa ‘wamefulia’, yaani anaepata laki moja, milioni moja na hata milioni tano kwa mwezi bado wote wanaimba wimbo ule ule unapfika mwisho wa mwezi!!

broke

  Kama sasa hivi unapata laki tano kwa mwezi, unaweza kufikiria ukipata milioni mbili kwa mwezi ndio maisha yatakuwa sawa, ila kuna anaepata hiyo milioni mbili na bado mambo yanazidi kuwa magumu kwake.

  Kwa maana hii basi fedha sio tatizo, yaani kama sasa hivi unapata fedha kidogo ila matatizo hayaishi basi hata ukipewa fedha nyingi kiasi gani ndio utakuwa umezidishiwa hayo matatizo. Fedha sio tatizo, tatizo kubwa ni wewe, na tatizo kubwa ni tabia zako linapokuja swala la fedha.

  Kuna baadhi ya tabia ambazo watu wengi wanazo na tabia hizo zinaleta matatizo mengi ya kifedha. Baadhi ya tabia hizo ni;

1. Manunuzi yasiyo ya msingi na yasiyo ya ratiba. Kuna watu wakishakuwa na fedha tu mfukoni chochote kitakachopitishwa mbele yake na kushawishiwa kununua anajikuta ameshanunua. Hii tabia wanayo sana kinadada/mama. Umewahi kufatwa na mtu anaefanya biashara akakushawishi kununua kitu anachouza na ukajiridhisha kununua ila unafika nyumbani na kugundua umefanya makosa kununua hicho kitu? Hiyo ni tabia ambayo inabidi uiangalie ili kuepuka matumizi mabovu ya fedha. Nunua vitu kutokana na mahitaji na sio kwa sababu umeona.

kununua

2. Kununua vitu ili kunekana wa daraja fulani. Kuna watu wengi sana wanaonunua vitu ambavyo havina uhitaji mkubwa kwenye maisha yao ila kutaka tu nao wavimiliki, kwa mfano simu za bei ghali, magazi ya bei ghali na nguo za bei ghali. Kama kuna uwezekano wa kupata kitu bora kwa bei ambayo sio kubwa sana na kikaweza kutimiza mahitaji yako basi nunua hicho. Kama wewe ni mtafutaji ni muhimu sana kuelewa hili ili kutojikuta kwenye wakati mgumu.

3. Hesabu mbaya za fedha. Kuna watu ukiwauliza gharama zao za maisha kwa mwezi mzima ni shilingi ngapi hata hawajui, labda na wewe ni mmoja wao! Kwani wewe kwa mwezi unatengeneza shilingi ngapi na matumizi yako ni shilingi ngapi? Watu wengi hawana bajeti ya matumizi yao yote kwa mwezi hivyo hujikuta wanatumia tu fedha mpaka zinapokwisha na mambo yanaanza kuwa magumu.

4. Tabia zilizokomaa(uteja), kuna watu ni wateja wa tabia fulani ambazo zinagharimu fedha nyingi sana, baadhi ya tabia hizo ni uchezaji kamari, unywaji wa pombe, utumiaji wa madawa na starehe mbalimbali. Kamari na michezo mingine inayofanana na hiyo(kama promosheni za mitandao ya simu) ni tabia ambazo zinawagharimu watu fedha nyingi sana. Unywaji wa pombe na starehe hizi ndio tatizo sana, kuna watu wameshajijengea tabia kwamba hawawezi kulala mpaka wanywe bia kadhaa. Hushangai baa kila siku zinaongezeka mitaani!!

addictive

5. Kuingia kwenye madeni bila ya kujua vizuri gharama za madeni hayo. Uelewa mdogo kuhusu mambo ya fedha hasa viwango vya riba umewafanya wengi kuchukua mikopo bila kujua gharama halisi za mkopo huo. Mwishowe mtu anakuja kuumia kwenye kulipa.

  Hizo ni baadhi tu ya tabia zinazokusababishia matatizo, na sio fedha. Badili kwanza tabia yako ndipo utamani kungeza kipato chako. Ukijaribu kuongeza kipato kabla ya kubadili tabia matatizo yatakuwa makubwa zaidi  ya uliyonayo kwa sasa.

TATIZO SIO FEDHA, TATIZO NI WEWE…..

  Ukiangalia matatizo uliyonayo, na malengo yako kwenye maisha jibu rahisi unalopata ni ukipata kiasi fulani cha fedha baasi, matatizo bai bai. Au unafikiri ukiweza kulipwa ama kutengeneza kiasi fulani kwa mwezi matatizo kwako ndio mwiko!!

pesa

  Kabla hujajiridhisha na jibu kwamba matatizo yote yanatokana na kukosa fedha fikiria hivi kwanza. Umewahi kugundua kwamba watu wengi huwa wanaishiwa fedha sawa licha ya kuwa na vipato tofauti? Kwa mfano wafanyakazi wengi kila inapokaribia mwisho wa mwezi(kuanzia tarehe ishirini na) wanakuwa ‘wamefulia’, yaani anaepata laki moja, milioni moja na hata milioni tano kwa mwezi bado wote wanaimba wimbo ule ule unapfika mwisho wa mwezi!!

broke

  Kama sasa hivi unapata laki tano kwa mwezi, unaweza kufikiria ukipata milioni mbili kwa mwezi ndio maisha yatakuwa sawa, ila kuna anaepata hiyo milioni mbili na bado mambo yanazidi kuwa magumu kwake.

  Kwa maana hii basi fedha sio tatizo, yaani kama sasa hivi unapata fedha kidogo ila matatizo hayaishi basi hata ukipewa fedha nyingi kiasi gani ndio utakuwa umezidishiwa hayo matatizo. Fedha sio tatizo, tatizo kubwa ni wewe, na tatizo kubwa ni tabia zako linapokuja swala la fedha.

  Kuna baadhi ya tabia ambazo watu wengi wanazo na tabia hizo zinaleta matatizo mengi ya kifedha. Baadhi ya tabia hizo ni;

1. Manunuzi yasiyo ya msingi na yasiyo ya ratiba. Kuna watu wakishakuwa na fedha tu mfukoni chochote kitakachopitishwa mbele yake na kushawishiwa kununua anajikuta ameshanunua. Hii tabia wanayo sana kinadada/mama. Umewahi kufatwa na mtu anaefanya biashara akakushawishi kununua kitu anachouza na ukajiridhisha kununua ila unafika nyumbani na kugundua umefanya makosa kununua hicho kitu? Hiyo ni tabia ambayo inabidi uiangalie ili kuepuka matumizi mabovu ya fedha. Nunua vitu kutokana na mahitaji na sio kwa sababu umeona.

kununua

2. Kununua vitu ili kunekana wa daraja fulani. Kuna watu wengi sana wanaonunua vitu ambavyo havina uhitaji mkubwa kwenye maisha yao ila kutaka tu nao wavimiliki, kwa mfano simu za bei ghali, magazi ya bei ghali na nguo za bei ghali. Kama kuna uwezekano wa kupata kitu bora kwa bei ambayo sio kubwa sana na kikaweza kutimiza mahitaji yako basi nunua hicho. Kama wewe ni mtafutaji ni muhimu sana kuelewa hili ili kutojikuta kwenye wakati mgumu.

3. Hesabu mbaya za fedha. Kuna watu ukiwauliza gharama zao za maisha kwa mwezi mzima ni shilingi ngapi hata hawajui, labda na wewe ni mmoja wao! Kwani wewe kwa mwezi unatengeneza shilingi ngapi na matumizi yako ni shilingi ngapi? Watu wengi hawana bajeti ya matumizi yao yote kwa mwezi hivyo hujikuta wanatumia tu fedha mpaka zinapokwisha na mambo yanaanza kuwa magumu.

4. Tabia zilizokomaa(uteja), kuna watu ni wateja wa tabia fulani ambazo zinagharimu fedha nyingi sana, baadhi ya tabia hizo ni uchezaji kamari, unywaji wa pombe, utumiaji wa madawa na starehe mbalimbali. Kamari na michezo mingine inayofanana na hiyo(kama promosheni za mitandao ya simu) ni tabia ambazo zinawagharimu watu fedha nyingi sana. Unywaji wa pombe na starehe hizi ndio tatizo sana, kuna watu wameshajijengea tabia kwamba hawawezi kulala mpaka wanywe bia kadhaa. Hushangai baa kila siku zinaongezeka mitaani!!

addictive

5. Kuingia kwenye madeni bila ya kujua vizuri gharama za madeni hayo. Uelewa mdogo kuhusu mambo ya fedha hasa viwango vya riba umewafanya wengi kuchukua mikopo bila kujua gharama halisi za mkopo huo. Mwishowe mtu anakuja kuumia kwenye kulipa.

  Hizo ni baadhi tu ya tabia zinazokusababishia matatizo, na sio fedha. Badili kwanza tabia yako ndipo utamani kungeza kipato chako. Ukijaribu kuongeza kipato kabla ya kubadili tabia matatizo yatakuwa makubwa zaidi  ya uliyonayo kwa sasa.

Posted at Thursday, July 25, 2013 |  by Makirita Amani

1 comments:

USIACHE KUWEKA MAONI YAKO HAPA.

  Duniani kuna watu wengi na wengi wamepita vizazi na vizazi. Katika watu hao wengi wachache sana wanajua ni nini waliletwa kufanya duniani. Wengi wamepita na wachache sana waliweza ama wameweza kukamilisha sehemu kidogo ya maisha yao hapa duniani.

  Kuna uwezekano mkubwa sana hata wewe hujui umekuja kufanya nini duniani, kama hujui sio kosa lako ila ukimaliza kusoma hapa na bado ukashindwa kutimiza lengo lako hapa duniani basi utakuwa na tatizo kubwa. Usiseme umeletwa duniani kuishi, hata chura anaishi, je thamani yako wewe ni sawa na chura? Kuna sababu kubwa ya wewe kuwa hapa duniani na kwa bahati nzuri leo inaweza kuwa siku muhimu sana kwenye maisha yako kwa kujua sababu hiyo.

MABADILIKOMABADILIKO2

  Tumeletwa duniani kufanya mabadiliko baasi, hakuna la ziada. Tofauti kubwa na uwezo ulionao wewe mwanadamu tofauti na wanyama wengine wanaoishi kama wewe ni wewe kuweza kuleta mabadiliko. Kama huleti mabadiliko yoyote utakuwa na tofauti gani na wanyama wengine?

  Ili kuweza kuleta mabadiliko cha kwanza ni kubadili hali iliypo, sheria, uelewa, ujuzi, na mitazamo ya watu. Huwezi kufanya mabadiliko kwa kufuata sheria zilizowekwa ama mitazamo iliyopo. Ni lazima uende mbele zaidi ya viwang vilivyowekwa ili kuweza kuwaonesha watu vitu ambavyo wamezuiwa kuviona, kwa kutokujua kama vipo ama vinawezekana. Naposema uvunje sheria simaanishi uende ukaibe ama ufanye uhalifu, hapana, namaanisha uende zaidi ya pale watu walipokubaliana ni kikomo.

  Ugunduzi wote unaotokea duniani unatokana na watu kuenda zaidi ya kipimo. Kama watu wangeridhika na kiwango kilochokuwepo enzi hizo mpaka sasa tungekuwa tunatumia zana za mawe, kusingekuwa na kompyuta, vyombo vya usafiri na vingine vingi ambavyo vimegunduliwa miaka ya hivi karibuni.

oldnewoldnew2

  Karne ya kumi na saba(wakati huo utawala wa Roma ukiwa na nguvu) mwanafalsafa na mnajimu Galileo Galilei alikwenda kinyume na utawala wa Roma. Roma iliweka sheria kwamba Dunia imesimama katikati na jua ndio linazunguka dunia. Kwa hiyo jua linachomoza asubuhi na linatua jioni(ndivyo inavyoonekana hivyo kwa mawazo rahisi kila mtu atakubali). Galileo baada ya kufanya majaribio mbali mbali aligundua kwamba jua ndio limesimama kati kati na dunia inalizunguka jua. Utawala wa Roma ulipopata habari zake alihukumiwa kifungo cha maisha kwa kwenda kinyume na sheria(nadhani unajua nguvu ya utawala wa roma kipindi hiko). Galileo hakukubali kubadili ugunduzi wake kwa sababu ya sheria hivyo alifungwa mpaka alipofia jela. Baadae sana ilikuja kugundulika ni kweli aliyoyasema Galileo.

galileogalileo2(GALILEO AKIHUKUMIWA)

  Kwa mfano huo wa Galileo (ipo mingine mingi sana) inaonesha ni jinsi gani watu wanaweza kuwa wagunduzi kwa kutkubaliana na hali iliyopo. Na pia hali iliyopo inawalemaza wengi kutofikiri kubadili hali.

  Hakikisha unaanza leo safari ya kuleta mabadiliko duniani. Usikubali kupita tu hivihivi bila kuacha alama yoyote. Kwa uwezo na kipaji cha pekee ulichonacho unaweza kufanya makubwa sana yatakayoweza kuisaidia dunia. AMKA NA UFANYE MABADILIKO.

UNAJUA ULICHKUJA KUFANYA DUNIANI?

  Duniani kuna watu wengi na wengi wamepita vizazi na vizazi. Katika watu hao wengi wachache sana wanajua ni nini waliletwa kufanya duniani. Wengi wamepita na wachache sana waliweza ama wameweza kukamilisha sehemu kidogo ya maisha yao hapa duniani.

  Kuna uwezekano mkubwa sana hata wewe hujui umekuja kufanya nini duniani, kama hujui sio kosa lako ila ukimaliza kusoma hapa na bado ukashindwa kutimiza lengo lako hapa duniani basi utakuwa na tatizo kubwa. Usiseme umeletwa duniani kuishi, hata chura anaishi, je thamani yako wewe ni sawa na chura? Kuna sababu kubwa ya wewe kuwa hapa duniani na kwa bahati nzuri leo inaweza kuwa siku muhimu sana kwenye maisha yako kwa kujua sababu hiyo.

MABADILIKOMABADILIKO2

  Tumeletwa duniani kufanya mabadiliko baasi, hakuna la ziada. Tofauti kubwa na uwezo ulionao wewe mwanadamu tofauti na wanyama wengine wanaoishi kama wewe ni wewe kuweza kuleta mabadiliko. Kama huleti mabadiliko yoyote utakuwa na tofauti gani na wanyama wengine?

  Ili kuweza kuleta mabadiliko cha kwanza ni kubadili hali iliypo, sheria, uelewa, ujuzi, na mitazamo ya watu. Huwezi kufanya mabadiliko kwa kufuata sheria zilizowekwa ama mitazamo iliyopo. Ni lazima uende mbele zaidi ya viwang vilivyowekwa ili kuweza kuwaonesha watu vitu ambavyo wamezuiwa kuviona, kwa kutokujua kama vipo ama vinawezekana. Naposema uvunje sheria simaanishi uende ukaibe ama ufanye uhalifu, hapana, namaanisha uende zaidi ya pale watu walipokubaliana ni kikomo.

  Ugunduzi wote unaotokea duniani unatokana na watu kuenda zaidi ya kipimo. Kama watu wangeridhika na kiwango kilochokuwepo enzi hizo mpaka sasa tungekuwa tunatumia zana za mawe, kusingekuwa na kompyuta, vyombo vya usafiri na vingine vingi ambavyo vimegunduliwa miaka ya hivi karibuni.

oldnewoldnew2

  Karne ya kumi na saba(wakati huo utawala wa Roma ukiwa na nguvu) mwanafalsafa na mnajimu Galileo Galilei alikwenda kinyume na utawala wa Roma. Roma iliweka sheria kwamba Dunia imesimama katikati na jua ndio linazunguka dunia. Kwa hiyo jua linachomoza asubuhi na linatua jioni(ndivyo inavyoonekana hivyo kwa mawazo rahisi kila mtu atakubali). Galileo baada ya kufanya majaribio mbali mbali aligundua kwamba jua ndio limesimama kati kati na dunia inalizunguka jua. Utawala wa Roma ulipopata habari zake alihukumiwa kifungo cha maisha kwa kwenda kinyume na sheria(nadhani unajua nguvu ya utawala wa roma kipindi hiko). Galileo hakukubali kubadili ugunduzi wake kwa sababu ya sheria hivyo alifungwa mpaka alipofia jela. Baadae sana ilikuja kugundulika ni kweli aliyoyasema Galileo.

galileogalileo2(GALILEO AKIHUKUMIWA)

  Kwa mfano huo wa Galileo (ipo mingine mingi sana) inaonesha ni jinsi gani watu wanaweza kuwa wagunduzi kwa kutkubaliana na hali iliyopo. Na pia hali iliyopo inawalemaza wengi kutofikiri kubadili hali.

  Hakikisha unaanza leo safari ya kuleta mabadiliko duniani. Usikubali kupita tu hivihivi bila kuacha alama yoyote. Kwa uwezo na kipaji cha pekee ulichonacho unaweza kufanya makubwa sana yatakayoweza kuisaidia dunia. AMKA NA UFANYE MABADILIKO.

Posted at Thursday, July 25, 2013 |  by Makirita Amani

0 comments:

USIACHE KUWEKA MAONI YAKO HAPA.

  Kwenye ulimwengu wa sasa ni muhimu sana kuwa jasiri ili kuweza kufikia malengo uliyojiwekea. Kukosa ujasiri ni sababu kuu ya watu wengi kushindwa kutimiza ndoto zao.

  Ujasiri ni muhimu sana kufikia mafanikio yako kwa sababu unakufanya uweze kutumia ujuzi, uwezo na vipaji vyako katika mazingira yoyote. Ujasiri ndio unawasaidia watu wengi ambao hawana uzoefu ila wanaweza kuanza mwanzo na mwisho wa siku wakawa wazoefu waliobobea.

ujasiri4ujasiri5

  Ujasiri ni kiashiria kwamba unajua unachokifanya na una imani kwamba utafikia malengo yako. Ujasiri ndio unakusaidia kutoyumbishwa na walimwengu.

Njia tano za kuongeza ujasiri na kufikia mafanikio.

1. Kaa na watu ambao wana mtizamo chanya, wanaojua ni nini wanataka kwenye maisha na wanafurahia maisha yao. Watu hawa ni jasiri na wako tayari kubadili sehemu ya maisha yao ambayo hawaifurahii. Ujasiri unaambukizwa, hivyo ukizungukwa na watu jasiri hata wewe utakuwa jasiri.

ujasiri2ujasiri6

2. Kila siku fanya kitu ambacho kinakufurahisha na kukufanya utabasamu. Kufurahia maisha kunaongeza ujasiri kwa sababu utaendelea kufanya yale yanayokufurahisha na mwisho wake ni kuyafikia mafanikio

3. Zingatia malengo na mipango yako. Tumia muda wako mwingi kuangalia kule unakokwenda na kuna jinsi maisha yako atakavyozidi kuwa mazuri kwa wewe kufikia malengo yako, hii itakupa ujasiri mkubwa na kuweza kuyafikia malengo haraka.

4. Usikate tamaa unapshindwa. Sio mara zote mambo yanatokea kama ulivyopanga, hivyo usikate tamaa na kujiona umeshindwa. Tofauti kati ya waliofanikiwa na walishindwa ni jinsi walivyopokea na kuvishinda vikwazo.

5. Tumia muda wako vizuri inapokuja kwenye kutimiza malengo yako. Hakikisha unafanya kile ulichopanga kwa muda uliopanga, kufanikiwa kwenye mambo madogo madogo kama kuweza kukamilisha ratiba kunakujengea ujasiri.

ujasiriujasiri7

  Majasiri ndio wanaofanikiwa kwenye jambo lolote wanalofanya, waoga hushindwa kabla hata ya kushindwa. Ujasiri ndio unamfanya mtu kuweza ku ‘take risk’  na ‘risk takers’ ndio wanaleta mabadiliko duniani. Usiwe mwoga tena jenga ujasiri wako na uyafurahie maisha yako.

NJIA TANO ZA KUONGEZA UJASIRI WAKO

  Kwenye ulimwengu wa sasa ni muhimu sana kuwa jasiri ili kuweza kufikia malengo uliyojiwekea. Kukosa ujasiri ni sababu kuu ya watu wengi kushindwa kutimiza ndoto zao.

  Ujasiri ni muhimu sana kufikia mafanikio yako kwa sababu unakufanya uweze kutumia ujuzi, uwezo na vipaji vyako katika mazingira yoyote. Ujasiri ndio unawasaidia watu wengi ambao hawana uzoefu ila wanaweza kuanza mwanzo na mwisho wa siku wakawa wazoefu waliobobea.

ujasiri4ujasiri5

  Ujasiri ni kiashiria kwamba unajua unachokifanya na una imani kwamba utafikia malengo yako. Ujasiri ndio unakusaidia kutoyumbishwa na walimwengu.

Njia tano za kuongeza ujasiri na kufikia mafanikio.

1. Kaa na watu ambao wana mtizamo chanya, wanaojua ni nini wanataka kwenye maisha na wanafurahia maisha yao. Watu hawa ni jasiri na wako tayari kubadili sehemu ya maisha yao ambayo hawaifurahii. Ujasiri unaambukizwa, hivyo ukizungukwa na watu jasiri hata wewe utakuwa jasiri.

ujasiri2ujasiri6

2. Kila siku fanya kitu ambacho kinakufurahisha na kukufanya utabasamu. Kufurahia maisha kunaongeza ujasiri kwa sababu utaendelea kufanya yale yanayokufurahisha na mwisho wake ni kuyafikia mafanikio

3. Zingatia malengo na mipango yako. Tumia muda wako mwingi kuangalia kule unakokwenda na kuna jinsi maisha yako atakavyozidi kuwa mazuri kwa wewe kufikia malengo yako, hii itakupa ujasiri mkubwa na kuweza kuyafikia malengo haraka.

4. Usikate tamaa unapshindwa. Sio mara zote mambo yanatokea kama ulivyopanga, hivyo usikate tamaa na kujiona umeshindwa. Tofauti kati ya waliofanikiwa na walishindwa ni jinsi walivyopokea na kuvishinda vikwazo.

5. Tumia muda wako vizuri inapokuja kwenye kutimiza malengo yako. Hakikisha unafanya kile ulichopanga kwa muda uliopanga, kufanikiwa kwenye mambo madogo madogo kama kuweza kukamilisha ratiba kunakujengea ujasiri.

ujasiriujasiri7

  Majasiri ndio wanaofanikiwa kwenye jambo lolote wanalofanya, waoga hushindwa kabla hata ya kushindwa. Ujasiri ndio unamfanya mtu kuweza ku ‘take risk’  na ‘risk takers’ ndio wanaleta mabadiliko duniani. Usiwe mwoga tena jenga ujasiri wako na uyafurahie maisha yako.

Posted at Thursday, July 25, 2013 |  by Makirita Amani

0 comments:

USIACHE KUWEKA MAONI YAKO HAPA.

© 2013 AMKA MTANZANIA. WP Theme-junkie converted by BloggerTheme9
Blogger templates | Distributed By: BloggerBulk Proudly Powered by Blogger.
back to top